Kobbie Mainoo ameiambia Manchester United anataka kuondoka kwa mkopo kutafuta nafasi ya kucheza mara kwa mara, lakini klabu hiyo inamtaka kiungo huyo wa England mwenye umri wa miaka 20 abaki na apiganie nafasi yake. (Athletic)
Wolves wako tayari kukataa ofa ya tatu ya Newcastle ya pauni £60m kwa ajili ya Jorgen Strand Larsen na bado wanasisitiza kuwa mshambuliaji huyo wa Norway mwenye umri wa miaka 25 hatauzwa katika dirisha hili la usajili. (Telegraph)
Tottenham wako karibu kukubaliana juu ya mkataba wa takriban pauni £60m na RB Leipzig kwa kiungo mshambuliaji wa Uholanzi, Xavi Simons, 22, baada ya kujitahidi kupunguza tishio la Chelsea kuharibu mpango wao. (Telegraph)


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni