Manchester United na Newcastle zote zinamtazama mshambuliaji wa Chelsea na Senegal Nicolas Jackson, 24, kama mchezaji mpadala iwapo watamkosa mshambuliaji wa RB Leipzig raia wa Slovenia, Benjamin Sesko, 22. (The Athletic)
Aston Villa pia wanamtaka mshambuliaji wa Manchester United ya Uingereza Ollie Watkins, 29, iwapo Mashetani Wekundu watashindwa kukamilisha dili la kumnunua Sesko. (Teamtalk)
RB Leipzig wamewasiliana na Liverpool kuhusu uwezekano wa kumsajili kiungo wa kati wa Uingereza Harvey Elliott, 22, huku Reds wakitaka pauni milioni 40 pamoja na chaguo la kumnunua tena, au zaidi ya pauni milioni 50 bila ya chaguo la kuweza kumnunua tena. (The Athletic)
Manchester United imekataa ofa tano kutoka vilabu vya Ligi Kuu England (Ligi ya Premia) na Italia kwa ajili ya beki wa Uingereza Harry Maguire, 32. (Mail)
Juventus wako tayari kumuuza beki wa kati wa Uingereza Lloyd Kelly, 26, na kumsajili mlinzi wa Arsenal Jakub Kiwior, 25, kama mbadala wake. (Gazzetta dello Sport)
#chanzobbcswahili


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni