Breaking

Jumanne, 9 Septemba 2025

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMANNE: LIVERPOOL YAMZUIA FEDERICO CHIESA KUONDOKA

 

Liverpool haina nia ya kumuuza Federico Chiesa licha ya kumuacha nje ya kikosi chake cha Ligi ya Mabingwa. Klabu ya Besiktas ya Uturuki ilikuwa imeonyesha nia ya kutaka kumsajili mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 27. (Liverpool Echo)

Kipa wa Ujerumani Stefan Ortega, 32, sasa anaweza kusalia Manchester City angalau hadi Januari baada ya Trabzonspor, klabu ya Uturuki ambayo alikuwa ikimfuatilia, kuamua kumsajili mchezaji wa kimataifa wa Cameroon Andre Onana mwenye umri wa miaka 29 wa Manchester United badala yake. (Manchester, Evening News)

Arsenal wako mstari wa mbele kumsajili kiungo wa Stuttgart Angelo Stiller baada ya ofa ya dakika za mwisho kutoka kwa Manchester United kukataliwa katika msimu wa kiangazi, lakini Bayern Munich na Real Madrid pia wanavutiwa na mchezaji huyo wa kimataifa wa Ujerumani, 24. (Express)

#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni: