Dkt Jane Goodall, mtafiti wa sokwe anayeaminika kuwa na ujuzi mpana na wa kina juu ya viumbe hao kuliko mtu mwingine yeyote yule amefariki dunia, akiwa na umri wa miaka 91.
Taasisi yake ya Jane Goodall Institute imesema Dkt Goodall alifariki kifo cha kawaida akiwa Calfornia nchini Marekani akiwa katika ziara yake ya kutoa mihadhara nchini humo.
Dkt Goodall alianza taaluma yake nchini Tanzania, huko Gombe Mkoani Kigoma mnamo mwaka 1960 akiwa na umri wa miaka 26 tu.
Utafiti wake ulifanya mapinduzi makubwa duniani katika kuzifahamu tabia za Sokwe kwa namna ambayo haikuwahi kufahamika hapo kabla.
#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni