Arsenal wanatathmini ofa ya kumnunua kiungo wa kati wa Uingereza Morgan Rogers, 23, lakini Aston Villa wanasema watamuuza Rodgers kwa ofa ya pauni milioni 80 pekee. (Sun),
RB Leipzig wamekubali makubaliano ya kibinafsi na kiungo wa kati wa Liverpool na England walio chini ya umri wa miaka 21 Harvey Elliott, 22, huku kiungo wa kati wa Uholanzi Xavi Simons, 22, akikaribia kukamilisha uhamisho wa kwenda Chelsea. (Florian Plettenberg)
Marseille wana nia ya kumsajili beki wa kushoto wa Ugiriki Kostas Tsimikas, 29, ambaye anatarajiwa kuondoka Liverpool msimu huu wa joto. (Footmercato - In French}
Mshambulizi wa Manchester United na Denmark Rasmus Hojlund, 22, na kambi yake wameweka wazi kwa Napoli na RB Leipzig kuwa anapendelea kuhama kwa mkopo na makubaliano ya kumnunua. (Fabrizio Romano)


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni