Breaking

Jumatano, 3 Desemba 2025

TRUMP ATAHUDHURIA DROO YA KOMBE LA DUNIA 2026


 Ikulu ya Marekani imethibitisha kwamba, Rais Trump atahudhuria hafla ya droo ya upangaji wa makundi ya Kombe la Dunia 2026, itakayofanyika mjini Washington mwishoni mwa wiki hii. Marekani itashiriki fainali hizo kama mwenyeji pamoja na Canada na Mexico.


“Ijumaa hii, Rais Trump atahudhuria hafla ya droo ya upangaji wa makundi ya Kombe la Dunia kwenye ukumbi wa Kennedy Center,” amesema Katibu wa Habari wa Ikulu, Karoline Leavitt, katika mkutano na waandishi wa habari.


Kombe la Dunia limepewa umuhimu mkubwa katika utawala wa Trump pamoja na sherehe za miaka 250 ya uhuru wa Marekani.


Hata hivyo, tukio hilo kubwa la michezo halijakwepa matatizo ya kisiasa kutokana na msimamo mkali wa Trump katika masuala kadhaa.

Hakuna maoni: