Bayern Munich wameulizia kuhusu upatikanaji wa mshambuliaji wa Senegal, Nicolas Jackson, 24, ambaye Chelsea wanataka pauni £48m ili kumuuza, anasakwa na Newcastle United. (Sky Sports Germany)
Mshambuliaji wa Newcastle, Alexander Isak, hatacheza mechi za maandalizi ya msimu dhidi ya Espanyol na Atletico Madrid mwishoni mwa hii kutokana na kutokuwa na uhakika juu ya mustakabali wake, anataka kwenda Liverpool. (Mail)
AC Milan wana nia ya kumchukua Rasmus Hojlund kutoka Manchester United. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 anapatikana kwa takriban pauni £30m lakini Milan wanataka kumchukua kwa mkopo. (Gazzetta dello Sport)
Tottenham wamekataliwa ofa ya pauni £30m kwa ajili ya kumsajili Nico Paz na Como, ambao thamani ya kiungo mshambuliaji huyo wa Argentina mwenye miaka 20 ni pauni £52m. (Sky Sports Italia)
Aston Villa wamekataa ofa ya pauni £18m kutoka Everton kwa ajili ya kiungo wa Scotland, John McGinn, 30, ambaye pia anaivutia klabu ya Newcastle. (Sky Sports News)


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni