Real Madrid ina nia ya kumsajili beki wa Tottenham Micky van de Ven, 24, lakini Spurs watafikiria kumuuza beki huyo wa Uholanzi kwa takriban £70m. (Fichajes - kwa Kihispania,)
Kiungo wa Manchester United na England Kobbie Mainoo, 20, huenda akafufua tena nia yake ya kujiunga na Napoli kwa mkopo mwezi Januari ikiwa hatapata muda zaidi wa kucheza Old Trafford. (ESPN)
Arsenal itazingatia mauzo ya mshambuliaji wa Brazil Gabriel Jesus, 28, na mshambuliaji wa Ubelgiji Leandro Trossard, 30, katika uhamisho wa Januari. (Football Insider)
#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni