Breaking


Jumanne, 23 Desemba 2025

UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI KITUNDA RELINI KUKAMILIKA KWA WAKATI - DC MPOGOLO

Mkuu wa wilaya ya ilala Edward Mpogolo, amewakikishia wakazi wa kata ya kitunda na kata jirani kukamilika kwa ujenzi wa shule ya sekandari ya kitunda relini kabla ya muda wa mkataba wa ujenzi huo.

Ametoa kauli iyo wakati wa ziara ya Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu -TAMISEMI  Reuben Kwagilwa, alipofanya ziara ya siku moja wilayani Ilala, katika jimbo la Kivule kwa  kutembelea miradi mbalimbali ya maendeleo katika sekta ya elimu na miundombinu ya barabara.

Mkuu huyo wa wilaya ya  ilala, Edward Mlogolo, amebainisha kuwa  ujenzi huo ulianza mwezi Septemba 2024 kwa mkataba wa muda wa miezi 18 lakini hadi kufikia sasa mradi huu umefika zaidi ya asilimia 96.

Huku akitumia nafasi hiyo, kumshukuru sana  Rais Dokta Samia Suluhu Hassan, kwa uwezeshaji huo na viongizi wanaamini mradi umetekelezwa ndani ya mwaka mmoja na  wanathibitisha matumizi mazuri ya muda na thamani ya walipa kodi za Watanzania. 

Hakuna maoni: