Aliyekuwa mkuu wa ujasusi nchini Saudia Turki al-Faisal alizua hisia kwenye mitandao ya kijamii kwa makala iliyowashutumu viongozi wa nchi za Magharibi kwa "viwango viwili" katika misimamo yao dhidi ya Iran, Israel na tishio la silaha za nyuklia.
Katika makala yake kwenye tovuti ya The National news, Al-Faisal anasema: "Ikiwa tungeishi katika ulimwengu ambamo haki inaenea, tungeona ndege za kivita za Marekani aina ya B-2 zikinyesha mvua ya mawe ya mabomu kwenye kinu cha Dimona na maeneo mengine ya nyuklia ya Israel."
Anaongeza, "Israel inamiliki mabomu ya nyuklia, na hivyo kukiuka Mkataba wa Kuzuia Uenezaji wa Nyuklia. Haijawahi kutia saini mkataba huo ili kuepuka uangalizi wa IAEA. Hakuna anayekagua vituo vyake vya nyuklia."
Anasema wale wanaohalalisha "shambulio la upande mmoja la Israel" dhidi ya Iran kwa kutaja wito wa viongozi wa Iran "kuiangamiza Israel" wanapuuza kauli za Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu, tangu alipoingia madarakani mwaka 1996, na wito wake wa mara kwa mara wa "kuiangamiza serikali ya Iran."
Al-Faisal anasema kwamba "unafiki wa nchi za Magharibi na uungaji mkono wao kwa Israel katika shambulio lake dhidi ya Iran ulitarajiwa. Pia 'wanailinda Israel katika mashambulizi yake yanayoendelea Palestina,'" hata kama baadhi yao wameondoa uungaji mkono huo.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni