Wizara ya Haki za Kijamii ya Uhispania imeitaka ofisi ya mwendesha mashtaka wa nchi hiyo kumchunguza winga wa Barcelona Lamine Yamal baada ya kuripotiwa kuwaajiri watu wenye ulemavu wa ngozi ili kutumbuiza kwenye sherehe yake ya kutimiza miaka 18.
Yamal aliandaa sherehe hiyo Jumapili katika nyumba iliyokodishwa huko Olivella, mji mdogo ulio kilomita 50 kaskazini magharibi mwa Barcelona, na wageni wakiwemo WanaYouTube, washawishi, na wachezaji wenzake kadhaa wa Barcelona.
Inadaiwa Yamal alikodisha kikundi cha watumbuizaji walio na unyonge, jambo ambalo Chama cha Watu wenye ‘Achondroplasia’ na ‘Dysplasias’ nyingine za Mifupa nchini Uhispania (ADEE) kilieleza kuwa halikubaliki katika karne ya 21.
“ADEE imewasilisha malalamiko, kwa hivyo wizara hii imeitaka ofisi ya mwendesha mashtaka kufanya uchunguzi ili kuona ikiwa sheria imekiukwa, haki za watu wenye ulemavu zizingatiwe,” Wizara ya Haki za Kijamii ya Uhispania imeliambia shirika la habari la AFP.
Taarifa ya wizara imesema: “Vitendo hivyo vinakiuka sio tu sheria za sasa lakini pia maadili ya kimsingi ya jamii inayotaka kuwa na usawa na heshima.
“Sheria ya jumla juu ya haki za watu wenye ulemavu inakataza kwa uwazi vitendo vifuatavyo: Maonyesho au shughuli za burudani ambazo watu wenye ulemavu au hali zingine hutumiwa kuchochea dhihaka, au kejeli kutoka kwa umma kwa njia inayopingana na heshima inayostahili utu ni marufuku,” imesema sehemu ya taarifa.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni