Vilabu viwili vinavyoongoza kwenye Ligi Kuu ya Saudi Arabia vinataka kumsajili Antony kutoka Manchester United huku uwezekano wa kurejea Real Betis, ambako winga huyo wa Brazil mwenye umri wa miaka 25 alicheza kwa mkopo msimu uliopita, ukiwa mdogo (Sky Sports).
Beki wa kushoto wa England Luke Shaw pia yuko tayari kusikiliza ofa kutoka vilabu vya Saudi Arabia huku akiwa tayari kuondoka Manchester United baada ya misimu 11 akiwa Old Trafford. Shaw ana umri wa miaka 30 (Sun).
Manchester United wamekataliwa ombi lao la mkopo kwa ajili ya kipa wa Aston Villa na Argentina Emiliano Martinez mwenye umri wa miaka 32 (Sun).
Newcastle United wanamtaka mshambuliaji wa Wolves raia wa Norway mwenye umri wa miaka 25, Jorgen Strand Larsen, kama mbadala wa mshambuliaji wa Sweden Alexander Isak, 25, endapo ataondoka msimu huu wa kiangazi (Express & Star).

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni