Breaking

Jumatatu, 14 Julai 2025

TETESI ZA SOKA ULAYA: GARNACHO AKATAA KUHAMIA KLABU YA NASSR


 Winga wa Manchester United Alejandro Garnacho amekataa kuhamia klabu ya Al Nassr, ya Saudia huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Argentina mwenye umri wa miaka 21 akipendelea kuhamia Ulaya. (Telegraph)

Bayern Munich inatarajiwa kuelekeza mawazo yake kwa mshambuliaji wa Arsenal na Ubelgiji Leandro Trossard, 30, ikiwa haitafanikiwa kumsajili winga wa Liverpool Luis Diaz, 28. (Bild - kwa Kijerumani)

Mshambuliaji wa Brighton Evan Ferguson amekubali kuhamia Roma, huku klabu hiyo ya Italia ikiwa kwenye majadiliano kuhusu ada ya mshambuliaji huyo wa Jamhuri ya Ireland mwenye umri wa miaka 20. (Gianluca di Marzio - kwa Kiitaliano)

Hakuna maoni: