Manchester United ina mpango wa kumsajili kipa wa England Nick Pope, 33, endapo Newcastle itakamilisha dili la kumsajili mlinda lango wa Southampton 27 Aaron Ramsdale, 27. (Sportsport)
Newcastle imekubaliana na Southampton kumsajili Ramsdale kwa mkopo na chaguo la kufanya mkataba huo kuwa wa kudumu mwishoni mwa msimu huu. (Athletic - usajili unahitajika)
Manchester United pia ina nia ya kumsajili mlinda lango wa Paris St-Germain na Italia Gianluigi Donnarumma, lakini inasita kujitosa kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 na Manchester City . (Sun)
#chanzobbcswahili

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni