Leo tarehe 30 Julai 2025, ulimwengu unaadhimisha Siku ya Urafiki Duniani (International Day of Friendship), siku maalum iliyoanzishwa na Umoja wa Mataifa kwa lengo la kuimarisha mshikamano, uelewano, na amani kupitia uhusiano wa kirafiki.
Katika dunia yenye changamoto za migogoro, chuki, na mgawanyiko, urafiki wa kweli ni silaha ya maelewano, tiba ya upweke, na chanzo cha matumaini. Siku hii hutufundisha kuwa tofauti zetu haziwezi kutuzuia kuwa marafiki,iwe ni tofauti za kabila, dini, rangi au mataifa. nzawadi ya maish
💬 UJUMBE MAALUM KWA WASOMAJI WETU
Leo ni siku nzuri ya:
• Kumkumbuka rafiki yako aliyekuwa nawe wakati mgumu
• Kutuma ujumbe wa upendo na shukrani
• Kuomba msamaha na kurejesha uhusiano uliopotea
• Kujenga urafiki mpya bila chuki wala mashaka.
📸 SHIRIKI URAFIKI WAKO MTANDAONI
Madelemo News inawatakia wasomaji wake wote Siku Njema ya Urafiki!
Kumbuka: Rafiki wa kweli ni hazina ya maisha. Thamini, linda, na heshimu urafiki wako.




Hakuna maoni:
Chapisha Maoni