Breaking


Jumanne, 26 Agosti 2025

TETESI ZA SOKA JUMANNE: JACKSON KUTUA BAYERN, MAINO KUTIMKA UNITED

 

Chelsea imekubali kumtoa kwa mkopo mshambuliaji wa Senegal mwenye umri wa miaka 24 Nicolas Jackson kwenda Bayern Munich. (Bild)

Kiungo wa England Kobbie Mainoo, 20, atafikiria kuondoka Manchester United katika wiki ya mwisho ya dirisha la usajili iwapo klabu itapokea ofa inayofaa. (Talksport)

Crystal Palace wamewasilisha ofa ya pauni milioni 15 kwa ajili ya kumnunua beki wa Uswizi wa Manchester City Manuel Akanji, 30. (Sun)

Mshambuliaji wa Denmark wa Manchester United Rasmus Hojlund, 22, atapata ongezeko kubwa la mshahara iwapo atakubali kujiunga na Napoli kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Gazzetta dello Sport)


Tottenham wanaweza kukosa mchezaji wa nne baada ya Como kukataa ofa ya pauni milioni 50 kutoka Spurs kwa ajili ya kiungo wa Argentina mwenye umri wa miaka 20 Nico Paz. (Mirror)


#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni: