Newcastle wanajiandaa kwa Liverpool kurejea na dau jipya la kati ya pauni milioni 120-130 kumnunua fowadi wao wa Uswidi Alexander Isak, 25. (Teamtalk), kutoka nje.
Wolves wanakabiliwa na vita vya kumbakisha mshambuliaji wa Norway Jorgen Strand Larsen, huku Newcastle wakishinikiza kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25 kwa takriban pauni milioni 60. (Express and the Star}
Manchester United wamefahamisha Napoli kwamba wako tayari kumtoa Mshambuliaji wao raia wa Denmark Rasmus Hojlund, 22 kwa mkopo au kupitia makubaliano ya kumuuza kabisa. (Fabrizio Romano)
Everton wana nia ya kumsajili beki wa Manchester City na Uholanzi Nathan Ake, 30, ili kuimarisha safu yao ya ulinzi. (Mail)
#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni