Breaking


Jumatatu, 18 Agosti 2025

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATATU: MAN UNITED WAMLENGA KIUNGO WA CRYSTAL PALACE

 

Manchester United wanafikiria iwapo watawasilisha ombi la kumnunua kiungo wa kati wa Crystal Palace na Uingereza Adam Wharton, 21. (Talksport).

Inter Milan wamekataa dau la euro 50m (£43m) kutoka kwa Chelsea kumnunua mlinzi wa Italia Alessandro Bastoni, 26. (La Gazzetta dello Sport)

Kiungo wa kati wa RB Leipzig na Uholanzi Xavi Simons, 22, ameiambia klabu hiyo kwamba anataka uhamisho wa kwenda Chelsea, licha ya kutakiwa na Bayern Munich na Manchester City. (ESPN)

AC Milan wana nia ya kusukuma dili la euro 35m (£30.2m) kwa mshambuliaji wa Denmark na Manchester United Rasmus Hojlund, 22, lakini pia wanamfikiria fowadi wa Juventus na Serbia Dusan Vlahovic, 25, kama mbadala wake. (La Gazzetta dello Sport)

Beki wa kulia wa Manchester City na England Rico Lewis, 20, anasema hana nia ya kuondoka katika klabu hiyo licha ya Nottingham Forest kumtaka. (Mail)

#ChanzoBbcswahili


Hakuna maoni: