Breaking


Jumapili, 7 Septemba 2025

BUKOBA VIJIJI WAMWAGA SHANGWE MAPOKEZI YA CCM






Maelfu ya wananchi wa Jimbo la Bukoba Vijijini wamefurika katika mkutano wa kampeni wa Mgombea mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dk Emmanuel Nchimbi uliofanyika katika eneo la Katoro mkoani Kagera. Wananchi hao walikuwa wakishangilia ahadi za ilani ya CCM huku wakiahidi ifikapo Oktoba 29 mwaka huu kura zao ni kwa CCM waweze kunufaika na miradi mbalimbali ya maendeleo.

Hakuna maoni: