Breaking

Jumapili, 21 Septemba 2025

𝗞𝗔𝗧𝗜𝗕𝗨 𝗠𝗞𝗨𝗨 𝗗𝗞𝗧. 𝗠𝗜𝗚𝗜𝗥𝗢 𝗔KI𝗦𝗔𝗟𝗜𝗠𝗜𝗔𝗡𝗔 𝗡𝗔 𝗪𝗔𝗡𝗔𝗖𝗛𝗜 𝗪𝗔 𝗠𝗕𝗜𝗡𝗚𝗔

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Asharose Migiro amepokea salamu za upendo kutoka kwa  maelfu ya wananchi waliojitokeza kwa wingi  Mbinga Mjini mkoani Ruvuma kwa ajili ya kumsubiria, kumlaki na kumsikiliza Mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM, Rais Dkt. 𝗦𝗮𝗺𝗶𝗮 𝗦𝘂𝗹𝘂𝗵𝘂 𝗛𝗮𝘀𝘀𝗮𝗻 leo tarehe 21 Septemba 2025.

Wananchi hao wameonesha shangwe na furaha yao kwa Katibu Mkuu na kumpa salamu zao za upendo wao wa dhati kwa Rais Dkt. Samia huku wakisema kuwa leo watampa maua yake ya kijani na njano kama ishara ya kumpitisha kwao bila kupingwa. 

Hakuna maoni: