Beki wa Crystal Palace Marc Guehi, 25, amewafahamisha washauri wake kwamba anapendelea kujiunga na Real Madrid baada ya uhamisho wake wa kujiunga na Liverpool kugonga mwamba. (Mirror)
Barcelona wamemtambua mshambuliaji wa Manchester City Erling Haaland, 25, kama mbadala wa muda mrefu wa mshambuliaji Robert Lewandowski. (Football Insider)
Mabingwa wa Ligi ya Primea, Liverpool wanamfuatilia kiungo wa Brighton Carlos Baleba. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Cameroon mwenye umri wa miaka 21 pia bado analengwa na Manchester United. (Team Talk)
#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni