Mshambuliaji wa Manchester City Erling Haaland amekuwa kivutio kikuu kwa rais wa Barcelona Joan Laporta, ambaye ana uhakika mchezaji huyo wa kimataifa wa Norway, 25, atajiunga na klabu hiyo ya La Liga siku zijazo. (El Nacional - In Spanish),
Manchester City wako tayari kushindana na Liverpool kwa ajili ya kumsajili bila malipo mlinzi wa England na Crystal Palace Marc Guehi mwenye umri wa miaka 25 msimu ujao, mkataba wake utakapokamilika. (Mirror)
Brentford wameonyesha nia ya kutaka kumnunua beki wa pembeni wa Borussia Dortmund mwenye umri wa miaka 19 Almugera Kabar. (Bild - In Deutch, Subscription Required)
#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni