Bayern Munich wamempiga bei kiungo wa kati wa Ufaransa Michael Olise mwenye umri wa miaka 23 kwa pauni milioni 100 huku Liverpool na vilabu vingine vikubwa vya Ulaya vikiwa na nia ya kutaka. kumnunua (Football Insider)
Chelsea wanatafuta kumsajili beki wa Crystal Palace Muingereza Marc Guehi, 25, na kipa wa AC Milan na Ufaransa Mike Maignan, 30, kwa uhamisho wa bila malipo msimu ujao. (TBR Football)
Manchester City hawana uwezekano wa kumwongezea mkataba kiungo wa kati wa Ureno Bernardo Silva, na hivyo kufungua njia kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 31 kuondoka kwa uhamisho wa bil amalipo msimu ujao, huku Juventus na Benfica zikionyesha nia. (AS - In Spanish)
#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni