Breaking

Jumatatu, 8 Septemba 2025

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATATU: MARC GUEHI HATAJIUNGA NA LIVERPOOL

 

Klabu ya Liverpool haitamsajili beki wa Crystal Palace Marc Guehi mwezi Januari. The Reds walishindwa kupata pauni milioni 35 za kumsajili mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza mwenye umri wa miaka 25 wiki iliyopita. Mkataba wake utakapokamilika msimu ujao wa kiangazi. (Times - usajili unahitajika)

Majadiliano kati ya mlinzi wa Liverpool na Ufaransa Ibrahima Konate kuhusu kandarasi mpya bado yanaendelea na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26 ambaye anaongoza orodha ya wachezaji wanaolengwa na Real Madrid. (Fabrizio Romano via Givemesport)

Mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 26, amemuomba Mohamed Salah wa Liverpool kuungana naye Real Madrid. Winga huyo wa Misri, 33, alitia saini mkataba mpya wa miaka miwili Anfield mwezi Aprili lakini huenda akaingiwa na tamaa ya kuhamia Bernabeu. (Teamtalk)

#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni: