Breaking


Jumapili, 12 Oktoba 2025

MAN UTD WANAVUTIWA NA WHARTON WA PALACE - TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI

 

Manchester United wanamfuatilia kwa karibu Adam Wharton, Reds hawatamchukulia Thomas Tuchel kama mbadala wa Ruben Amorim, Vinicius Junior kumfungulia njia Erling Haaland huko Real Madrid.

Adam Wharton, 21, analengwa na Manchester United. Mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza anapendwa sana Old Trafford na klabu hiyo inaweza kutoa ofa ya pauni milioni 60 kumnunua kiungo huyo wa Crystal Palace. (Mirror)

Wakati huo huo, United haitamchukulia meneja wa England Thomas Tuchel kama mbadala anayeweza kushika nafasi hiyo iwapo watamtimua Ruben Amorim. (Sun)


Bayern Munich wamedhamiria kuongeza mkataba wa beki Dayot Upamecano, 26, huku Liverpool ikivutiwa naye, licha ya klabu hiyo ya Ujerumani kushindwa kukubaliana nyongeza ya ofa ya mlinzi huyo wa kati ambaye anaweza kuondoka bila malipo mwezi Juni 2026. (Florian Plettenberg)


#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni: