Breaking

Jumamosi, 25 Oktoba 2025

TETESI ZA SOKA JUMAMOSI: CHELSEA, LIVERPOOL ZAMTAKA UPAMECANO

 

Chelsea inaweza kuokoa pauni milioni 52 ikiwa haitamsajili beki wa kati wa Ufaransa Dayot Upamecano hadi msimu ujao wa joto atakapokuwa mchezaji huru, lakini kuna hatari ya kumkosa mchezaji huyo wa miaka 26 iwapo Bayern Munich itamuuza Januari, huku Liverpool ikiwa miongoni mwa vilabu vinavyomtaka. (Football.London)

Licha ya kiungo wa kati wa Sporting, Denmark, Morten Hjulmand, 26, kuwa na kifungu cha kutolewa cha pauni milioni 70, Manchester United wana imani kwamba wanaweza kumpata kwa takriban pauni milioni 50. (Teamtalk)

Manchester United pia inamfuatilia kiungo wa kati wa Bayern Munich na Ujerumani Aleksandar Pavlovic, 21. (Caught Offside)


#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni: