Manchester City wanapanga dau la pauni milioni 75 kumnunua kiungo wa kati wa Nottingham Forest Elliot Anderson msimu ujao wa joto lakini kuna uwezekano wakakabiliwa na ushindani mkali kutoka kwa Chelsea kumnunua mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza, 22. (Express)
Tottenham wanajiandaa kuchukua hatua kali ya kumrejesha Harry Kane kaskazini mwa London kutoka Bayern Munich msimu ujao wa joto na wako tayari kutimiza masharti ya kutolewa kwa nahodha huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 32 na mahitaji ya mshahara. (TeamTalks,)
Crystal Palace wametulia kuhusu mustakabali wa Adam Wharton huku kukiwa na uvumi unaoongezeka kutoka kwa wapinzani wa Premier League Manchester United kutaka kumnunua kiungo huyo wa kati wa Uingereza mwenye umri wa miaka 21. (Sky Sports)
Kocha mkuu wa Chelsea Enzo Maresca ana mashaka juu ya mustakabali wake wa muda mrefu Stamford Bridge huku Juventus ikimfikiria Muitaliano huyo mwenye umri wa miaka 45 kama mgombea makini wa kuinoa klabu hiyo ya Serie A. (TeamTalks)
#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni