Mkurugenzi wa michezo wa Bayern Munich Max Eberl anasema winga wa Ufaransa mwenye umri wa miaka 23 Michael Olise, ambaye amekuwa akihusishwa na vilabu kadhaa, hana kipengele cha kutolewa katika mkataba wake, ambao utaendelea hadi Juni 2029. (Talksport)
Newcastle United wanatathmini uwezekano wa kumrejesha kiungo wa kati wa Uingereza Elliot Anderson, 22, kwenye klabu, baada ya kumuuza kwa Nottingham Forest mwaka jana. (i Paper - usajili unahitajika)
Manchester United bado wana nia ya kumsajili kiungo wa Ujerumani Angelo Stiller, 24, lakini ada itakayotolewa na klabu ya Stuttgart kwa mchezaji huyo wa miaka 24 inatarajiwa kuwa zaidi ya €50m (£43.5m). (Sky Sports Germany)
#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni