Breaking


Jumamosi, 24 Januari 2026

DKT. MWIGULU ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO YA MSIBA WA MZEE EDWIN MTEI

Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Nchemba akitia saini kitabu cha maombolezo ya msiba wa  aliyekuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT), marehemu Mzee Edwin Isaac Mtei, Nyumbani kwa marehemu Tengeru (Chama), Wilaya ya Arumeru Mashariki mkoani Arusha, Januari 24, 2026. Dkt. Mwigulu ameongozana na Mkewe Neema Mwigulu.



Mheshimiwa Dkt. Mwigulu anamwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika mazishi hayo.

Mzee Edwin Mtei, ambaye aliwahi kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT) kuanzia mwaka 1966 hadi 1974, alifariki dunia usiku wa Januari 19, 2026, jijini Arusha.

Hakuna maoni: