Breaking


Jumapili, 4 Januari 2026

TRUMP ASIFU KUKAMATWA KWA NICOLAS MADURO


Rais wa Marekani, Donald Trump, amesifu kukamatwa kwa Rais wa Venezuela, Nicolás Maduro na Jeshi la Marekani, huku Mwanasheria Mkuu wake akiahidi kiongozi huyo wa Venezuela atakabiliwa na adhabu kali chini ya sheria za Marekani.

Maduro na Mke wake wote wanakabiliwa na mashtaka ya dawa za kulevya na ugaidi nchini Marekani, ambayo imeendesha kampeni ya shinikizo kwa miezi kadhaa dhidi ya rais huyo wa mrengo wa kushoto.

Kulingana na Mwanasheria Mkuu wa Marekani Pam Bondi, Maduro na Mke wake, Cilia Flores, wameshtakiwa katika Mahakama ya New York kwa makosa yanayojumuisha njama ya ugaidi wa dawa za kulevya, njama ya kuingiza kokaini, na mashtaka yanayohusiana na bunduki.

Hakuna maoni: