Breaking


Ijumaa, 10 Aprili 2026

MELANIA TRUMP AKANUSHA KUHUSIKA NA JEFFREY EPSTEIN, AITA TUHUMA “UZUSHI WA KUMCHAFOA SIFA”


Mke wa Rais Melania Trump amekanusha kuwa na uhusiano na Jeffrey Epstein, akiwaambia waandishi wa habari katika Ikulu ya White House kwamba madai yoyote yanayowaunganisha wawili hao "yanahitaji kumalizika haraka".

Katika tangazo la kushtukiza siku ya Alhamisi, mke wa rais alitoa wito wa vikao vya bunge kwa ajili ya manusura wa biashara haramu ya ngono iliyoendeshwa na Epstein.

Pia alikanusha uvumi mtandaoni kwamba Epstein alimtambulisha kwa Donald Trump, akiuita "majaribio ya kikatili ya kunichafulia sifa".

Haijulikani ni nini kilisababisha atoe tangazo hilo.

Hakukuwa na dalili yoyote kutoka ofisini kwake kwamba atatoa taarifa kuhusu Epstein, na Ikulu ya White House haikushirikisha mada hiyo mapema.

Alisema hakuwa mwathirika wa Epstein, ambaye "alikutana naye" kwa muda mfupi tu mwaka wa 2000.

"Sijawahi kuwa na ufahamu wowote kuhusu unyanyasaji wa Epstein dhidi ya waathiriwa wake," alisema. "Sijawahi kushiriki katika nafasi yoyote. Sikuwa mshiriki."

Pia alikana kumjua Ghislaine Maxwell, mshirika wa Epstein aliyefungwa jela.

Hakuna maoni: