Breaking


Jumatano, 13 Mei 2026

MBUNGE KIGOMA MJINI CLEYTON CHIPANDO ATAKA KITENGO CHA ELIMU YA LISHE MITANDAONI

 


Mbunge wa Kigoma Mjini, Clayton Chipando, (Baba Levo) ameshauri Wizara ya Afya kuwa na Kitengo maalum kwa ajili ya kutoa elimu Afya ya Lishe Mitandaoni dhidi ya baadhi ya watu wanaotoa Elimu hiyo bila kuwa na mwongozo sahihi wa Wizara yenye dhamana ya Afya.

Mhe. Chipando ameyasema hayo Mei 12, 2026 jijini Dodoma wakati akichangia Hotuba ya Bajeti ya Wizara ya Afya kwa mwaka wa fedha 2026/27 

"Mhe. Mwenyekiti mimi nimekula Ugali kwa miaka 35, lakini Leo kila ukiingia mtandaoni utakutana na matangazo mbalimbali yanayotumika kuelimisha watu juu ya utaratibu wa matumizi ya chakula" amesema Mhe. Chipando

Mhe. Chipando amesema katìka siku za hivi karibuni kumekuwepo na wimbi la watoa huduma, ambao kwa namna moja au nyingine wamekuwa wakitoa elimu kuhusu lishe na kuwaweka wananchi kwenye mtanziko wa nini wale na kiwango gani.

Kwa upande wake Mhe. Khamis Ali Vuai Mbunge wa Jimbo la Mkwajuni (CCM) mkoani Kaskazini UngujaMbunge  aliyeomba kutoa taarifa wakati wa Mchango huo, aliliambia Bunge  kuwa taifa la India ni moja ya Taifa lililoweka Utaratibu wa nani atatoa elimu ya Afya, hivyo kama Taifa tuone kama kitu muhimu, jambo lililokubaliwa na Mchangiaji.

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limeendelea na Uchangiaji wa Bajeti ya Wizara ya Afya Fungu 52,  kwa mwaka wa fedha 2026/27 iliyowasilishwa Mei 11, 2026 Bungeni na Waziri wa Afya Mhe Mohamed Mchengerwa na kuomba kuidhinishiwa kiasi cha shilingi Trilioni 1.8 kwa ajili yakutekeleza vipaumbele 11.

Hakuna maoni: