Kupitia chapisho lililosambazwa kwenye mitandao ya kijamii, wadau wa soka wamealikwa kutoa maoni yao kwa kutaja jina moja la mchezaji wanayeamini atang’ara zaidi na kuiongoza timu yake kufikia mafanikio makubwa katika mashindano hayo.
Mjadala huo unatarajiwa kuendelea kwa siku 40 zijazo hadi kufikia Julai 20, siku ambayo mshindi wa tuzo mbalimbali za mashindano hayo atafahamika. Wachezaji kadhaa kutoka mataifa tofauti wamekuwa wakitajwa kutokana na kiwango bora walichoonyesha tangu kuanza kwa michuano hiyo.
Tuzo ya Mchezaji Bora wa Kombe la Dunia hutolewa kwa mchezaji aliyetoa mchango mkubwa zaidi ndani na nje ya uwanja kupitia uwezo wake, mabao, pasi za mabao na ushawishi wake kwa timu katika mashindano yote.
Swali kubwa linalobaki kwa sasa ni: Je, ni nani ataibuka kuwa Mchezaji Bora wa Kombe la Dunia mwaka huu? Mashabiki wanaendelea kutoa maoni yao huku wakisubiri kuona nani atakayethibitisha ubora wake hadi mwisho wa michuano.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni