Bohari ya Dawa (MSD) imeendelea kuthibitisha ubora wake katika usimamizi wa ununuzi wa umma baada ya kutunukiwa *Tuzo ya Utendaji Bora katika Ununuzi wa Umma** na Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA).
MSD imetambuliwa kama *Taasisi Bora kwa Ujumla katika Matumizi ya Mfumo wa Kitaifa wa Ununuzi wa Umma kwa Njia ya Kielektroniki (NeST)* kwa mwaka wa fedha *2025/2026*, ikiwa ni uthibitisho wa uwazi, ufanisi na matumizi sahihi ya teknolojia katika utekelezaji wa shughuli za ununuzi wa umma.
Tuzo hiyo ilikabidhiwa hapo jana tarehe *29 Julai 2026*, wakati wa *Kongamano la 10 la Kitaifa la Ununuzi wa Umma*, linaloendelea katika Ukumbi wa AICC, Mkoani Arusha.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni