Breaking


Jumapili, 27 Julai 2025

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI: MAN CITY NA MAN UTD WANAMTAKA DONNARUMMA

Manchester United na Manchester City zote zinavutiwa na mlinda mlango wa Paris St-Germain wa Italia Gianluigi Donnarumma, 26, huku timu hiyo ya Ligue 1 ikiwa tayari kumnunua kipa wa Lille Mfaransa Lucas Chevalier, 23, kama mbadala wake. (L'Equipe - in French)

Galatasaray pia wanatazamiwa kumtafuta Donnarumma, ambaye anakaribia kuingia mwaka wa mwisho wa mkataba wake huko Paris St-Germain. (Footmercato - in French)


Arsenal wanatumai kufikia dili la pauni milioni 60 kwa ajili ya Eberechi Eze wa Crystal Palace, huku mshambuliaji huyo wa Uingereza mwenye umri wa miaka 27 akitaka kuhamia katika kikosi cha Mikel Arteta. (Footmercato - in French)

Everton wako kwenye mazungumzo na Bayern Munich kuhusu uhamisho wa pauni milioni 7.8 kwa ajili ya beki wa kushoto wa Morocco Adam Aznou, 19. (Athletic - subscription required)


#Chanzobbcnewsswahili


 

Hakuna maoni: