Chama Cha Mapinduzi kimesema kitashinda Uchaguzi Mkuu wa Oktoba Mwaka huu kwa mujibu wa sheria na taratibu za kidemokrasia kwani hakuna sababu ya CCM kushindwa Visiwani Zanzibar .
Katibu wa Kamati Maalum ya Nec Zanzibar, Idara ya Itikadi, Uenezi na Mafunzo ,Khamisi Mbeto Khamis, ameeleza hayo baada ya mgombea Urais wa CCM, Rais Dk Hussein Ali Mwinyi alipohutubia maelefu ya wana CCM na Wananchi.
Mkutano wa Uzinduzi wa Kampeni za CCM kwa Zanzibar ,zimezinduliwa katika Uwanja wa Kumbukumbu ya Mwenyekiti Mao Tse Tung, Kisiwani Unguja.
Mbeto amesema Ushindi wa CCM hauna kizuizi chochote baada ya serikali ya Awamu ya Nane kutimiza wajibu wa kuwatumikia wananchi chini ya serikali ya Rais Dk Mwinyi.
Alisema haiba ya Ustawi wa Maendeleo inayoonekana Unguja na Pemba ,ni tiketi itakayokipatia Ushindi wa kishindo CCM Mwaka 2025-2030.
Aidha, Katibu huyo Mwenezi ,aliongeza kusema kwa CCM ni fahari kuona idadi kubwa ya Wananchi, wakiendelea kukiunga mkono , kukuamini , kukipenda na kukitegemea .
Katibu huyo Mwenezi akijigamba mbele ya Waandishi wa habari, amesifu kazi kubwa iliofanywa na SMZ, miaka mitano iliopita chini ya Utawala wa Dk Mwinyi.
Alisema CCM kitashinda kwa Asilimia 85 ya kura za Urais, hivyo Mgombea wake Dk Mwinyi , atarudishwa tena madarakani kwa ridhaa ya Wananchi .
Mbeto amesema kimsingi Utendaji wa Serikali ya Awamu ya Nane, umezikonga nyoyo za Wananchi pia kuwavutia hata wageni wanaotembelea Visiwani humu.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni