Breaking


Ijumaa, 12 Septemba 2025

ANAEKIMBIA KODI NI ADUI WA MAENDELEO-RC HALIMA

Mkuu wa Mkoa wa Singida, Mhe. Halima Dendegu amesema amewataka  wafanyabiashara na wananchi wa Singida  kuendelea kulipa kodi kwa hiari na kutoa taarifa  za ukwepaji kwani wakwepaji ndio maadui wa maendelea yanayoonekana nchini. 

Ameyasema hayo tarehe 11.09.2025 ofisini kwake alipokutana na Naibu Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Bw. Mcha Hassan Mcha aliembatana na viongozi wengine wa TRA alipotembelea ofisini kwake kwa lengo kumshukuru kwa ushirikiano anaondelea kuutoa kwa TRA katika ukusanyaji wa kodi.

Mhe. Halima amesema licha ya mafanikio makubwa katika ukusanyaji wa kodi na kuweza kuvuka malengo, ofisi yake imejipanga kuhakikisha mkoa wa Singida unaendelea kupiga hatua zaidi katika ukusanyaji wa kodi ili kuingia  katika mikoa mitatu bora katika kuchangia pato la taifa.

Hakuna maoni: