Breaking


Ijumaa, 5 Septemba 2025

TETESI ZA SOKA IJUMAA: MAGUIRE ANAWINDWA NA VILABU VYA SAUDI

 

Harry Maguire wa Manchester United na England, mwenye umri wa miaka 32, amekuwa akiwindwa na vilabu viwili vya Saudi Pro League na yupo tayari kufikiria uhamisho mwishoni mwa msimu huu. (Sun) 

Mlinda mlango wa timu hiyo pia, Onana naye ameruhusiwa kwenda Uarabuni.

Mwenyekiti wa Crystal Palace Steve Parish alifanya mazungumzo ya ana kwa ana na beki wa England Marc Guehi, 25, pamoja na familia yake baada ya kusitisha uhamisho wa pauni milioni 35 kuelekea Liverpool. (Mirror)

Liverpool wanapanga kufanya majaribio ya kumnasa Guehi Januari na pia wanamtazama mshambuliaji wa Bayern Munich na timu ya taifa ya Ufaransa Michael Olise, 23, kama mrithi wa muda mrefu wa nyota wao wa Misri Mohamed Salah, 33. (Mail)

Bayern Munich nao wameingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsajili Guehi, huku Real Madrid na Barcelona pia zikifuatilia kwa karibu suala lake. (Express)

#ChanzoBbcswahili


Hakuna maoni: