Nahodha wa Manchester United Bruno Fernandes, 30, bado anaweza kuhamia Saudi Arabia, Tottenham wanamtaka Morgan Rogers wa Villa, huku Arsenal wakikataa nia ya Uturuki kumnunua winga Leandro Trossard.
Kiungo wa kati wa Manchester United Bruno Fernandes, 30, alikataa ofa tatu kutoka kwa klabu za Saudi zinazomilikiwa na PIF msimu huu, huku mchezaji huyo wa kimataifa wa Ureno akichagua kusalia Old Trafford. Hata hivyo, nahodha huyo wa United bado ana uwezekano wa kwenda Saudi Arabia kwa sababu kuna nia ya kumsajili katika msimu wa joto wa 2026. (Talksport)
#ChanzoBbcswahili


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni