Breaking


Ijumaa, 17 Oktoba 2025

KINYEREZI YAFURIKA WANANCHI KWENYE MKUTANO WA KAMPENI CHATANDA AKIOMBA KURA ZA CCM.

Mratibu wa Kampeni za CCM Jijini DSM, na Mwenyekiti waJumuiya ya Umoja wa Wanawake wa Chama Cha Mapinduzi Tanzania (UWT) Ndg. Mary Pius Chatanda (MCC)  tarehe 16 Oktoba, 2025, afanya Mkutano wa Kampeni kwenye kata ya Kinyerezi Jimbo la Segerea na kuwaomba Wananchi kujitokeza kwa Wingi Oktoba 29, 2025 kwa Kumchagua Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, kumchagua Mgombea Ubunge wa Jimbo la Segerea Bonnah Kamoli, pamoja na Madiwani wote wa Kata ndani ya Jimbo la Segerea kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM)

Chatanda ameyasema hayo wakati akinadi Ilani ya CCM 2025/2030 na kuwaambia Wananchi kuwa Dkt. Samia anatosha na anafaa kuliongoza Taifa hili kwa kuwa ametekeleza kwa vitendo ilani ya CCM 2020/2025 kwa kukamilisha miradi Mbalimbali ya Kimaendeleo na kuifanya Tanzania kuwa Nchi ya Mfano kwa Mataifa Mbalimbali Duniani.









Akimuombea kura Mgombea Ubunge Jimbo la Segerea Bonnah Kamoli, pamoja na Madiwani wa Kata ndani ya jimbo la Segerea, Chatanda amewaomba wananchi wa Segerea kutofanya makosa bali kumchagua kwa kura nyingi ili azidi kuwaletea Maendeleo.

Hakuna maoni: