Breaking

Jumamosi, 4 Oktoba 2025

MAN UTD ITABIDI IFANYE UAMUZI JUU YA FERNANDES - TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI

 

Vilabu kutoka Saudi Arabia na Ulaya vinatazamiwa kuijaribu nia ya Manchester United kuendelea kumshikilia nahodha Bruno Fernandes mwezi Januari, Napoli wanaongoza katika mbio za kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United Kobbie Mainoo, huku Barcelona na Liverpool wakimtaka beki wa Bayern Munich Dayot Upamecano.

Azma ya Manchester United ya kumbakisha nahodha wao Bruno Fernandes, 31, inatazamiwa kuwa katika majaribu wakati wa dirisha dogo la usajili Januari huku vilabu vya Saudi Pro League na Ulaya vikimhitaji kiungo huyo wa kati wa Ureno. (Manchester Evening News)

Napoli wako mstari wa mbele kumsajili kiungo wa kati wa Manchester United na Uingereza Kobbie Mainoo, 20, mwezi Januari. (Tuttomercatoweb - in Italian)


#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni: