Breaking


Jumamosi, 18 Oktoba 2025

TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAMOSI: PALACE KUMUUZA MARC GUEHI MWEZI JANUARI

 

Crystal Palace wanapanga kumuuza mlinzi wa Uingereza Marc Guehi mwezi Januari na Liverpool haiko tena mstari wa mbele kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, huku Barcelona, ​​Real Madrid na Bayern Munich wakimtaka. (The I paper) 

Kiungo wa kati wa England na Crystal Palace Adam Wharton, 21, ndiye analengwa na Manchester United kwa uhamisho wa Januari, ingawa anaweza kugharimu takriban £70m. (Team talk) 

Liverpool na Chelsea zote zilikataliwa na Everton msimu wa joto baada ya kuonesha nia yao ya kumnunua mlinzi wa kati wa England Jarrad Branthwaite, 23. (Mail)


Tottenham na Liverpool wote wanamtaka winga wa Bournemouth na Ghana Antoine Semenyo, 25. (Talksport)


#ChanzoBbcswahili

Hakuna maoni: