Akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Victoria Falls Mhe. Waziri Kombo amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. CP Suzan S. Kaganda, pamoja na viongozi wa ngazi ya juu kutoka Tanzania na Zimbabwe. Ziara yake inafanyika kufuatia mwaliko rasmi kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara za Kimataifa wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Prof. Dkt. Amon Murwira.
Mkutano wa mwaka huu unaongozwa na kaulimbiu isemayo: “Innovation for Impact: Leveraging Technology and Collaboration for Future-Ready Societies” (Ubunifu kwa Matokeo: Kutumia Teknolojia na Ushirikiano kwa Jamii Zinazojitayarisha kwa Baadaye). Kaulimbiu hii inalenga kusisitiza umuhimu wa ubunifu, teknolojia na mshikamano wa kimataifa katika kujenga jamii imara kwa maendeleo ya baadaye.
Shughuli za siku ya kwanza zinajumuisha Kongamano la Biashara (Business Forum) linalokutanisha wafanyabiashara na wawekezaji kutoka nchi za Afrika na Nordic (Denmark, Finland, Iceland, Norway na Sweden), kwa lengo la kukuza fursa za biashara na uwekezaji baina ya pande hizo mbili.
Katika mkutano huo, Mhe. Waziri Kombo anatarajiwa kuwasilisha vipaumbele vya Serikali ya Awamu ya Sita katika nyanja za biashara, uwekezaji, elimu, teknolojia na maendeleo ya kijamii, sambamba na kuimarisha ushirikiano wa karibu kati ya Tanzania na nchi za Nordic.






Hakuna maoni:
Chapisha Maoni