Taarifa zilizothibitishwa na afisa mmoja wa klabu ya Don Bosco, aliyokuwa moja ya klabu alizohudumia Chico kabla ya kuhamia Yanga kutoka TP Mazembe, zinasema kuwa alifariki baada ya kuugua kwa siku chache tu.
“Alikuwa sawa kiafya wiki iliyopita, lakini hali yake ilibadilika katikati ya wiki hii. Alipopelekwa hospitali Jumatano, Desemba 11, hakuweza kurudi. Alikuwa sawa kabisa lakini ameugua siku kama tatu tu, na leo tumeambiwa amefariki,” amesema bosi huyo.
Chico alijiunga na Yanga Januari 22, 2022, akitokea TP Mazembe, katika kipindi kilichowezesha mchezaji mwingine, Mukoko Tomombe, kuhamia TP Mazembe.
Kifo cha Chico kimeacha pengo kubwa katika soka la Tanzania na DR Congo. Mashabiki wake wanamkumbuka kwa mchango wake uwanjani na tabia yake nzuri nje ya uwanja.
Hii ni fursa ya kuwakumbusha mashabiki wote thamani ya wachezaji waliokuwa mabalozi wa timu zao. Chico Ushindi atakumbukwa daima.


Hakuna maoni:
Chapisha Maoni