Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inatoa angalizo kwa wananchi, hususan wakazi wa Mkoa wa Ruvuma, kuchukua tahadhari kutokana na vipindi vifupi vya mvua kubwa vinavyotarajiwa katika maeneo machache ndani ya saa 24 zijazo. Wananchi wanashauriwa kuzingatia tahadhari dhidi ya athari zinazoweza kusababishwa na mvua hizo, ikiwemo mafuriko ya ghafla na usumbufu wa shughuli za kila siku.
Maeneo Yanayotarajiwa Kupata Hali ya Mawingu, Mvua na Ngurumo
• Mikoa ya Dodoma na Singida
• Kusini mwa Mkoa wa Morogoro
• Mikoa ya Kigoma, Tabora na Katavi
• Mikoa ya Kagera, Geita, Mwanza, Shinyanga, Mara na Simiyu
• Mikoa ya Rukwa, Songwe, Mbeya, Iringa, Njombe na Ruvuma
Maeneo haya yanatarajiwa kuwa na hali ya mawingu kiasi, mvua na ngurumo katika maeneo machache, pamoja na vipindi vya jua.
Mikoa ya Lindi na Mtwara
• Inatarajiwa kuwa na hali ya mawingu kiasi,
• Mvua katika maeneo machache,
• Pamoja na vipindi vya jua.
Maeneo ya Pwani na Kaskazini Mashariki
• Visiwa vya Unguja na Pemba
• Mikoa ya Tanga na Dar es Salaam
• Kaskazini mwa Mkoa wa Morogoro
• Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Manyara
• Mkoa wa Pwani (ikijumuisha Visiwa vya Mafia)
Maeneo haya yanatarajiwa kuwa na hali ya mawingu kiasi, mvua nyepesi katika maeneo machache, pamoja na vipindi vya jua.
TMA inaendelea kusisitiza wananchi kufuatilia taarifa rasmi za hali ya hewa na kuchukua tahadhari zinazostahili, hususan katika maeneo yenye uwezekano wa mvua kubwa kwa vipindi vifupi.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni