Breaking


Jumanne, 24 Machi 2026

ANGALIZO : MVUA KUBWA ZATARAJIWA KATIKA BAADHI YA MIKOA TANZANIA


 Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imetoa tahadhari ya uwepo wa vipindi vifupi vya mvua kubwa vinavyotarajiwa kunyesha katika maeneo machache ya mikoa ya Kigoma, Katavi, Tabora, Rukwa, Kagera, Mwanza, Geita, Shinyanga, Lindi, Mtwara, Tanga, Dar es Salaam, Morogoro, pamoja na Pwani ikijumuisha visiwa vya Mafia na vile vya Unguja na Pemba. 

Kwa ujumla, hali ya hewa kwa saa 24 zijazo kuanzia saa 3:00 usiku wa leo Machi 24, 2026, inatarajiwa kuwa ya mawingu yenye mvua na ngurumo katika maeneo machache, huku baadhi ya maeneo yakipata vipindi vya jua. 


Aidha, upepo wa pwani unatarajiwa kuvuma kwa kasi ya hadi kilomita 30 kwa saa kutoka Kusini Mashariki, na hali ya bahari kuwa na mawimbi madogo hadi makubwa kiasi. 


Wananchi wanashauriwa kuchukua tahadhari stahiki dhidi ya mvua hizo, huku matarajio yakionesha kuendelea kwa mvua katika maeneo mengi ya nchi ifikapo Alhamisi, Machi 26, 2026.

 

Hakuna maoni: