Kiungo mahiri Bruno Guimarães ameendelea kuwa gumzo kuhusu hatma yake ndani ya klabu ya Newcastle United, huku taarifa zikionyesha kuwa huenda akaendelea kusalia licha ya kuvutiwa na vigogo wa Manchester City na Manchester United.
Ingawa hapo awali pia aliwahi kuhusishwa na Arsenal, hali ya sasa ndani ya Newcastle inaonekana kuwa ngumu kuruhusu nyota wawili muhimu kuondoka kwa wakati mmoja, hasa ikizingatiwa uwezekano wa klabu hiyo kuuza kiungo Sandro Tonali ambaye bado ni kijana na ana thamani kubwa sokoni.
Hali hiyo inaifanya Newcastle kuwa makini zaidi katika maamuzi yao ya usajili, jambo linaloweza kumpa Guimarães nafasi kubwa ya kubaki St James’ Park msimu ujao.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni