Breaking


Jumatatu, 6 Aprili 2026

KANYE WEST ATIKISA SOFI STADIUM, AVUNA MABILIONI KUPITIA MAONYESHO MAWILI YALIYOUZWA YOTE


Msanii wa muziki wa rap, Kanye West, ameripotiwa kuingiza mapato makubwa kufuatia kufanikisha kufanya maonyesho mawili yaliyovunja rekodi kwa kuuzwa tiketi zote katika uwanja wa SoFi Stadium nchini Marekani.


Kwa mujibu wa taarifa kutoka Bloomberg, matamasha hayo mawili yalizalisha takribani dola milioni 33 za Kimarekani, sawa na zaidi ya shilingi za Kitanzania bilioni 86.5. Inaelezwa kuwa onyesho la Ijumaa pekee lilifanikiwa kuingiza zaidi ya dola milioni 18, takribani shilingi bilioni 47.3, kupitia mauzo ya tiketi.


Takwimu hizi zinaweka matamasha hayo katika orodha ya maonyesho yenye mapato makubwa zaidi katika historia ya muziki wa moja kwa moja, zikionesha wazi nguvu ya jina na mvuto wa Kanye West kwa mashabiki wake duniani kote.


Hata hivyo, pamoja na ukubwa wa takwimu hizo, bado hazijathibitishwa rasmi na wadau huru wa tasnia ya muziki, hali inayomaanisha kuwa makadirio yanaweza kutofautiana kulingana na vyanzo mbalimbali.


Hakuna maoni: