Serikali imesema itaendelea kuwekeza katika miradi ya barabara kwa kuwa ndiyo msingi wa kufungua uchumi, kurahisisha usafirishaji wa mazao na kuchochea maendeleo ya wananchi vijijini na mijini.
Hii ni kwa mujibu wa Waziri Mkuu, Dokta Mwigulu Nchemba, alipokagua ujenzi wa barabara ya Iringa, Ipogolo-Kilolo yenye urefu wa zaidi ya kilomita 33 kwa kiwango cha lami, na wenye thamani ya zaidi ya shilingi Bilioni-60 na umefikia asilimia 96.
Aidha, Waziri Mkuu, amesema Serikali imekubaliana kuhakikisha miradi yote iliyoanza inakamilishwa kwanza, sambamba na kuendelea kutoa fedha za utekelezaji kwa miradi iliyosainiwa mikataba lakini haikupata malipo ya awali.
Kwa upande wake, Mbunge wa Kilolo, Rita Kabati, amesema wananchi wa Kilolo wameendelea kunufaika na uwekezaji wa Serikali katika sekta ya miundombinu, huku akiishukuru Serikali kwa kuendelea kutatua changamoto za usafiri katika wilaya ya Kilolo.
Wananchi 596 waliopitiwa na mradi huo walilipwa fidia ya zaidi ya shilingi Bilioni-2, huku ajira 393 zikizalishwa, ambapo asilimia 95 ya ajira hizo zilitolewa kwa wananchi wa Ipogolo na Kilolo.





Hakuna maoni:
Chapisha Maoni