Kwa mujibu wa taarifa kutoka Africa CDC, takriban visa 246 vya maambukizi na vifo 65 vimeripotiwa katika miji ya uchimbaji wa dhahabu ya Mongwalu na Rwampara. Mamlaka za afya zinaendelea kufuatilia hali hiyo ili kuzuia kusambaa zaidi kwa ugonjwa huo hatari.
Ugonjwa wa Ebola uligunduliwa kwa mara ya kwanza mwaka 1976 nchini DRC, na wataalamu wanaeleza kuwa unaaminika kusambazwa kutoka kwa popo kwenda kwa binadamu. Huu ni mlipuko wa 17 wa Ebola kuripotiwa nchini humo.
Ebola husambazwa kupitia kugusana moja kwa moja na majimaji ya mwili wa mtu aliyeambukizwa. Ugonjwa huo unaweza kusababisha kutokwa damu, kuharibika kwa viungo vya mwili pamoja na matatizo makubwa ya kiafya endapo mgonjwa hatapatiwa huduma mapema.
Dalili za Ebola ni pamoja na homa kali, maumivu ya misuli, uchovu, maumivu ya kichwa na koo. Wataalamu wa afya wanasisitiza umuhimu wa kuchukua tahadhari, ikiwemo kunawa mikono mara kwa mara na kuepuka kugusana na wagonjwa wenye dalili za ugonjwa huo.

Hakuna maoni:
Chapisha Maoni